Kenya: Wabunge kujadili mapendekezo ya utafutaji haki dhidi ya wanajeshi wa Uingereza nchini humo
Wabunge wa Kenya wanatazamiwa kujadili ripoti inayopendekeza mashtaka ya mauaji dhidi ya wanajeshi waliozuru Kenya yafunguliwe katika mahakama za nchini humo.
Pendekezo hilo litakalojadiliwa siku ya Jumanne, limo katika ripoti ya timu ya bunge inayopitia mkataba wa ushirikiano wa ulinzi kati ya Kenya na Uingereza.
Inafuatia ghadhabu ya umma baada ya madai kwamba wanajeshi wa Uingereza huenda walihusika katika mauaji ya Agnes Wanjiru - mwanamke Mkenya aliyepatikana amekufa mwaka wa 2012 baada ya kutumia tafrija ya jioni na wanajeshi.
Inafuatia ghadhabu ya umma baada ya madai kwamba wanajeshi wa Uingereza huenda walihusika katika mauaji ya Agnes Wanjiru - mwanamke Mkenya aliyepatikana amekufa mwaka wa 2012 baada ya kuwa katika tafrija ya jioni na wanajeshi.
Jeshi la Uingereza lilishutumiwa kwa kuficha ukweli, kwa mujibu wa ripoti ya Sunday Times, lakini Wizara ya Ulinzi ya Uingereza baadaye ilisema inashirikiana na uchunguzi wa Kenya kuhusu kifo hicho.
Wabunge nchini Kenya walio katika kamati ya ulinzi pia wanapendekeza kwamba wanajeshi wanaozuru walazimike kuhudumia jamii kupitia uwajibikaji wa kijamii wa shirika.
Walikutana na maafisa wa ubalozi wa Uingereza, maafisa kutoka wizara ya ulinzi na mashauri ya kigeni ya Kenya, pamoja na wapelelezi wanaochunguza mauaji ya Bi Wanjiru kabla ya kuandika ripoti hiyo.
Jeshi la Uingereza lina kitengo cha kudumu cha kufaya mazoezi katika mji wa kati wa Nanyuki chini ya makubaliano na serikali ya Kenya.
Imepakiwa mnamo 17:1317:13
Polisi Tanzania: Thabo Bester na mpenzi wake kurejeshwa Afrika Kusini
w
GALLO imagesCopyright: GALLO images
Mhalifu maarufu wa Afrika kusini Thabo Bester na mpenzi wake Dr Nandipha Magudumana hawataendelea na kesi yoyote katika mahakama ya Tanzania, watashtakiwa katika mahakama za Afrika Kusini.
Msemaji wa Polisi wa Tanzania, David Misime ameiambia BBC kuwa Bester na mpenzi wake huyo waliingia nchini kinyume cha sheria, lakini kwa mujibu wa sheria za kimataifa watafata utaratibu wa kuwarudisha Afrika kusini ili waendelee na mashtaka yao.
“Baada ya polisi wetu kupata taarifa zake na anayedaiwa kuwa mpenzi wake Dk Nandipha. Walikamatwa na bado wapo kizuizini. Tunakamilisha taratibu za kisheria kati ya nchi hizo mbili na tutamkabidhi kwa maafisa wa Afrika Kusini.
Siku ya Jumamosi Polisi walithibitisha kukamatwa kwa Thabo Bester, mpenzi wake Dk. Nandipha Magudumana, na Zakaria Alberto huko Arusha, Kaskazini mwa Tanzania.
Bester ambaye anajulikana kama "mbakaji wa Facebook" kwa kutumia mtandao wa kijamii kuwarubuni waathiriwa wake.
Alipatikana na hatia mwaka wa 2012 kwa kumbaka na kumuua mpenziwe mwanamitindo Nomfundo Tyhulu. Mwaka mmoja mapema, alipatikana na hatia ya kubaka na kuwaibia wanawake wengine wawili.
Alifanikiwa kutoroka gerezani na kuaminisha mamlaka za Afrika kusini kuwa alijiua kwa moto katika chumba chake cha gereza.
Wakati huo huo, Askari wa gereza aliyesimamishwa kazi na baba yake mpenzi wa Thabo Bester wanakabiliwa na msururu wa mashtaka yakiwemo mauaji, uchomaji moto na kusaidia kutoroka kwa Thabo Bester.
Kulingana na stakabadhi za mahakama, watu hao wawili wanadaiwa kumuua kimakusudi mtu asiyejulikana Machi mwaka jana.
Kesi yao imeahirishwa hadi Aprili 17 kwa uwezekano wa maombi ya dhamana, Wamewekwa rumande ya polisi.
Kampuni ya ulinzi inayomilikiwa na Uingereza ya G4s ilikuwa ikiendesha gereza alimofungiwa Bester. Tangu wakati huo imechukuliwa na maafisa wa magereza ya Afrika Kusini kufuatia kashfa yake ya kutoroka.